Skip to main content

Ujenzi wa misingi ya uwekezaji

Kila aina ya uwekezaji ili uwe na tija ni lazima kwanza miundombinu muhimu ya kuuwezesha kufanya kazi iwepo, bila hivyo tutazidi kushuhudia mitaji mingi ikipotea, na tayari tumeshuhudia biashara nyingi na uwekezaji mwingi unafanyika lakini baada ya siku au miaka kadhaa yote inakufa, hii ni kutokana na kukosa kuandaa miundombinu itakayoendelea kuleta uhai kwenye uwekezaji, Ni lazima miundombinu ya msingi iandaliwe kama vile:

1. Kusuka mfumo imara wa kupata taarifa za muhimu na wakati wowote juu ya sekta unayohitaji kuwekeza.

2.Kuandaa/ kutengeneza watu sahihi watakao kusaidia katika kila hatua ya uwekezaji utayoifikia, kuna baadhi ya uwekezaji unahitaji kutumia watu wengi wenye ujuzi na uzoefu mbalimbali na watu hawa kila mmoja ana nafasi yake kulingana na hatua ya mradi ulipofikia

3. Kujijengea uwezo wa kiufahamu, maarifa na uelewa wa sekta husika, ni lazima utafute ujuzi wa kutosha juu ya sekta hiyo ikiwemo kufahamu, jinsi ya kuendesha na kuisimamia miradi hiyo, Changamoto zake, Muda wa mradi kuanza kuzalisha faida, soko, na hata kujua mustakabari wa sekta hiyoKwa leo tuishie hapa, ila kumbuka kama samaki anavyohitaji maji ili kuishi kadhalika na uwekezaji pia unavyohitaji kujengewa miundombinu imara ya kuiwezeha kuishi, katika hali halisi si jambo rahisi kuandaa miundombinu ya uwekezaji kwani inahitaji muda wa kutosha,utulivu,uvumilivu na akili za kutosha, na baadhi ya sekta zinahitaji kujitoa zaidi kuandaa miundombinu yake.

Kama waswahili wasemavyo maji hufuata mkondo kadhalika na Pesa nyingi na nzuri huifuata miradi iliyojengewa miundombinu imara.


By Allen Lupembe


Comments

Popular posts from this blog

Hatua tisa za kuanzisha biashara.

Kuanzisha biashara kunahitaji kupanga mipango, kufanya maamuzi ya kifedha  na kutimiza  taratibu kadhaa za kisheria.  Wakati mwingine sio lazima kuzifanya  hatua zote kwa wakati mmoja lakini kadri biashara inavyozidi kuimarika basi ni lazima uzitimize hizo hatua muhimu. Kuna baadhi ya hatua ambazo ni lazima uzifanye mwanzoni kabisa mwa biashara yako, vinginevyo biashara yako itakufa ingali bado changa au itasimamishwa na mamlaka husika za kisheria. Hatua zifuatazo zawaeza kukusaidia katika kupanga,kujiandaa na kuingoza biashara yako kwa ufanisi mkubwa zaidi: Andaa mwongozo wa biashara ( Business plan) Mwongozo huu utakusaidia  kukupa dira ya namna ya kuanza na kuendesha biashara yako kwa ufanisi. Tafuta msaada na mafunzo ya kibiashara Tumia fursa za bure za kujifunza  zinazopatikana mtandaoni au fursa za bei rahisi zinazotolewa katika makongamano ya ujasiriamali na uwekezaji hapa nchini. Chagua eneo sahihi la kuiweka biashara yako. Tafuta us

Mambo muhimu kuhusu mkopo - Sehemu ya 1

            Utangulizi  MKOPO ni kiwango cha fedha ambacho mtu hupewa na taasisi ya kifedha na kutakiwa kurudisha kiwango hicho kikiwa na riba kwa kipindi cha muda fulani. Mkopo unaweza  kuwa katika  mfumo wa bidhaa au kifaa lakini vitu hivyo  vyote hatimaye lazima thamani yake ipimwe na fedha,kwasababu  kazi kubwa ya fedha ni kupima thamani ya bidhaa au vifaa,mfano mtu anapochukua mkopo wa bidhaa zenye thamani ya Milioni kumi,tafsiri  yake ni kwamba umechukua mkopo wa Milioni kumi. Katika makala hii nitaeleza kuhusu mkopo kwa ujumla ingawa kwa sehemu kubwa nitaeleza juu ya mkopo wa fedha  unaotolewa na taasisi za za kifedha. Watu wamezoea kuwa mabenki ndiyo yanayo husika na utoaji wa mikopo tu lakini kiuhalisia kuna taasisi nyingi za kifedha zinazo husika na utoaji wa mikopo . Kulingana na sheria ya benki na taasisi za kifedha vyombo ambayo vinaruhusiwa na huduma ya utoaji mikopo ni benki ,saccos ,makampuni ya mikopo na mifuko ya hifadhi ya jamii. Tafiti zinaonyes

Mambo sita ya msingi kuhusu soko la bidhaa yako au huduma unayotoa

Sokoni ni eneo ambalo wauzaji wa bidhaa na wanunuzi wa bidhaa hukutana kubadilisha thamani vitu. Katika nyakati hizi soko la bidhaa linaweza kuwa ni kwa njia ya mtandao hivyo sio lazima mnunuzi na muuzaji wa bidhaa kukutana uso kwa uso. Kipindi hiki ni zama za sayansi na teknolojia ambazo zimetoa matumizi makubwa ya mtandao katika shughuli za mwanadamu hususani biashara hivyo kuna biashara nyingi zinafanyika kwenye mtandaoni (Online). Ninaamini wengi wetu tumeingia katika shughuli za ujaseriamali kwa dhumuni la kuongeza kipato hatimaye kuwa na maisha mazuri. Hivyo basi swala la soko katika biashara yako ni muhimu sana kwasababu bidhaa unazozalisha ni kwaajili ya kuuza na kupata faida.Katika biashara ya aina yoyote mzalishaji hana budi afahamu mambo kadhaa ya msingi kuhusu soko la bidhaa yake au huduma na kisha  kumsaidia kufanya maamuzi ya kumuwezesha kupata faida ya juu katika biashara anayoifanya. 1.Unahitaji kufanya utafiti wa kina juu ya soko la bidhaa z