Jinsi ya kupata wazo la biashara (Sehemu ya kwanza).


Changamoto walionayo watu wengi sio kuanzisha biashara au kuanzisha kampuni bali ni kuanzisha biashara gani au kampuni gani,kuna watu wanafedha lakini hawajui wafanye nini na fedha hizo. Watu wengi wamekutana na changamoto  hii ya kupata wazo la biashara kiasi ambacho wamekuwa wakitamani kufanya biashara lakini hawajui ni biashara gani haswa wanapaswa kufanya.

Napenda kukukaribisha kwa moyo mkunjufu katika  kusoma makala hii ambayo nitaeleza kwa uchache baadhi ya njia za kupata wazo la biashara au kuanzisha Kampuni.

CHANGAMOTO ZILIZOPO KATIKA JAMII UNAYOISHI

Chunguza katika jamii unayoishi je kuna changemoto gani au zipi na je kupitia changamoto hizo unaweza kufanya biashara gani au kuanzisha kampuni gani ambayo bidhaa zake zitakuwa ni suluhu ya hiyo changamoto katika jamii husika. Njia hii mara nyingi inakupa uhakika wa soko la bidhaa zako na huduma utakayotoa kwa wananchi. Kusudi la njia hii ni kutatua changamoto inayokabili jamii husika wakati ukiendelea kujiingizia kipato.

Mfano  I:- Katika kijiji cha WATANZANIA TUMEAMUA kuna changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama hivyo unaweza kuchimba kisima na kuanzisha biashara ya kuuza maji kwa wanakijiji.

Mfano II:- Katika kijiji cha KILA MTU ANA THAMANI  kuna changamoto kubwa ya upatikanaji wa usafiri hivyo unaweza kuanzisha huduma ya kutoa usafiri wakati huohuo unajitengenezea kipato.

Mfano III:- katika mtaa wa HEKIMA kuna changamoto ya upatikaji wa sehemu ya kula kwa wafanyakazi wa kiwanda cha TANZANITE YETU hivyo unaweza kuja kufanya biashara ya kuanzisha mgahawa na kuuza chakula kwa wafanyakazi wa kiwanda hicho na wanajamii wengine.

Mfano IV:- Katika kijiji cha MAARIFA YA MAISHA kuna changamoto ya upatikani wa bidhaa za matumizi ya nyumbani hivyo wananchi wanasafiri umbali mrefu kwenda kununua bidhaa hizo, hivyo basi kupitia chanagamoto hii unaweza kuanzisha baishara ya kuuza duka.

Mfano V:- Katika mtaa wa ELIMU NI MUHIMU  kuna changamoto ya upatikanaji wa mahitaji ya sokoni mfano nyanya ,vitunguu ,matunda n.k hivyo unaweza kuanzisha biashara ya kuuza bidhaa hizo katika eneo zuri na safi ambalo litawavutia wateja kuja kununua bidhaa zako.

MUHIMU 

Tafiti ni muhimu sana kabla ya kuazisha biashara yoyote ile, hivyo basi ninashauri ufanye utafiti wa kina juu ya eneo unaloishi ilikujua changamoto ambazo zinakabili jamii inayokuzunguka na kisha kuja na mpango mkakati wa kuanzisha biashara ambayo inakuwa suluhu ya hizo changamoto wakati wewe unajiingizia kipato.

Itaendelea sehemu ya pili

Imeandaliwa na James Albert 

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

Namna Ya Kuanzisha Biashara

Biashara Ya Mbao.

USIMAMIZI WA FEDHA KATIKA BIASHARA YAKO.