Kutengeneza pesa mtandaoni ni jambo ambalo linaweza kupunguza changamoto ya upungufu wa fursa za ajira nchini.
Kila mwaka mamia elfu ya vijana wanahitimu kutoka katika vyuo vya kati na vyuo vikao na kuingia katika soko la ajira nchini Tanzania.
Mambo Muhimu Ya Kijana Kuzingatia ili Kutengeneza kipato mtandaoni.
Chagua unahitaji kufanya nini
Ukweli ni kwamba huwezi kufanya kila kitu mtandaoni kwasababu fursa zipo nyingi sana.
Unahitaji kuchagua jambo ambalo unahitaji kufanya ili kutengeneza pesa mtandao.
Uchaguzi wako unatakiwa kutegemeana na utafiti ambao umeufanya ni ujuzi gani ambao unahitajika sokoni au ni bidhaa gani inahitajika sokoni
Mtaalamu wa mauzo ndugu Amos Nyanda anasema "Soko ni maabara hivyo halidanganyi"
Kumbuka huduma au bidhaa unayotaka kupeleka sokoni sio kwaajili yako hivyo ni busara soko liamue huduma gani au bidhaa gani inahitajika ili uweze kutengeneza pesa mtandaoni.
Kubali kujifunza
Ili uweze kuingiza kipato mtandao ni lazima uwe ni mtu ambaye uko tayari kujifunza kwasababu unaingia katika sehemu mpya. Jifunze namna mifumo inafanya kazi na kuleta matokeo yaani wekeza kwanza kujifunza utaratibu mzima wa mfumo wa mtandao husika.
Lakini mtandao ni sehemu ambayo mambo yanabadilika kila wakati.
Huwezi kukwepa mabadiliko hivyo namna pekee ya kwendana nayo ni kuamua kujifunza ili ukabiliana nayo.
Tafuta mtu wa kukuelekeza
Kuna watu ambao wapo kwenye mtandao kwa muda mrefu sana wanafanya jambo fulani mfano kwenye masuala ya blog ndugu Ally Msangi ni mtu ambaye anafanya masuala ya blogging kwa muda mrefu.
Hawa watu kwa jina lingine wanaitwa MENTORS .
Ni watu muhimu kwababu wanajua njia sahihi ambayo ukiipitia unaweza kupata matokeo mazuri.
Mentors ni watu wenye uzoefu wa kutosha kwasababu wanaishi jambo ambalo wanafundisha.
Usijifunze jambo kwa mtu ambaye yeye mwenye haishi hicho kitu mfano usijfunze masuala ya mauzo kwa mtu ambaye yeye sio muuzaji.
Ukijifunza kwa mentor itakupunguzia gharama ambayo ungeingia wakati unanunua vitabu na muda ambao ungetumia kujifunza huko mtandaoni kama YOUTUBE na majukwa mengine.
Kuwa mvumilivu
Huwezi kuingia mtandaoni leo na ukaanza kutengeneza pesa mtandaoni wakati huohuo inachukua muda. Unahitaji kuwa mvumilivu wakati unafanya kazi mtandaoni ili uweze kupata matokeo unayotarajia tofauti na hivyo.
Mwisho, kijana wekeza muda kujifunza kabla ya kufanya jambo lolote itakusaidia kuepuka makosa mengi, kupoteza pesa na muda wako pia.
Comments
Post a Comment