Skip to main content

Namna ya Kuingiza Pesa Mtandaoni.

  


Kuingiza pesa mtandaoni katika nyakati hizi za mapinduzi ya teknolojia kumekuwepo na hamasa kubwa ya watu kutengeneza pesa kupitia mtandao wa inteneti jambo ambalo sio baya lakini linahitaji mpango madhubuti.

Kuingiza pesa mtandaoni inawezekana kabisa kupitia jitihada makusudu.

Ukweli ni kwamba sio jambo jepesi, inahitaji kuwa mbunifu, bidii na ujuzu wa namna ya kuingiza pesa.

Baadhi hapa chini ni namna ya kuingiza pesa mtandaoni  

1. Namna ya kwanza unaweza kuingiza pesa kupitia blog kwa kuuza bidhaa ndani yake kama vitabu au course ambazo umetengeneza mwenyewe na kuuzia watu wengine.

2. Namna ya pili  ni  kuingia makubaliano na baadhi ya kampuni.

Hii itakupa fursa ya ili kutangaza bidhaa zao kupitia blog na wao wakakulipa commission fulani ambayo mmekubaliana nao ili uweze kuingiza pesa kupitia mtandao.

3. Namna ya tatu kuingiza pesa mtandaoni ni kutangaza aina ya huduma unayoweza kuwapa watu na wao waka tayari kulipia kupitia mtandao wako wa blog.

4. Unaweza ya nne  ni kujisajili katika makujwa ya wafanayakazi huru (freelancer).

Majukwa hayo ni kama upwork, fiverr na mengine mengi kisha ukauza ujuzi wako huko na kujiingizia fedha za kutosha.

5. Unaweza kutengeneza akaunti za mitandao ya kijamii na kisha kujitangaza kwa kutoa huduma fulani.

Mfano kutengeneza matangazo ya biashara (Copy Writing), unaweza kuanda poster kwaajili ya watu kutangazia biashara zao.

6. Unaweza kutengeneza pesa kupitia kusimamia na kuandika maudhui kwenye akaunti za watu kwaajili ya kutangaza biashara zao.

Kujibu maswali yote ambayo wateja wao wanauliza kupitia mitandao ya kijamii ya biashara husika.

Jambo muhimu ni kujenga ujuzi ambao unahitaji kuufanyia kazi sokoni katika kuingiza kipato ili iwe rahisi kwako kupata wateja.

Kwenye majukwa ya mtandao wanahitajika watu wenye ujuzi.

Namna zote ambazo nimeendika zitakazokusaidia kuingiza pesa mtandaoni zinahitaji ujuzi fulani

Niandikie unatamani kujifunza kuhusu nini  kwenye masuala ya ujasiriamali na biashara kwa ujumla.

 

Endelea kutembelea tovuti hiii kwaajili ya kujifunza zaidi kuhusu ujasiriamali na biashara.

Kwenye sehemu ya mitandao ya kijamii naomba nifollow ili uweze kupata mafunzo katika hizo sehemu pia.

Mwisho, suala la kufanya kazi mtandao ili kutengeneza kipato  linahitaji uwekezaji, uvumilivu na kufanya kazi kwa bidii.



Comments

Popular posts from this blog

Hatua tisa za kuanzisha biashara.

Kuanzisha biashara kunahitaji kupanga mipango, kufanya maamuzi ya kifedha  na kutimiza  taratibu kadhaa za kisheria.  Wakati mwingine sio lazima kuzifanya  hatua zote kwa wakati mmoja lakini kadri biashara inavyozidi kuimarika basi ni lazima uzitimize hizo hatua muhimu. Kuna baadhi ya hatua ambazo ni lazima uzifanye mwanzoni kabisa mwa biashara yako, vinginevyo biashara yako itakufa ingali bado changa au itasimamishwa na mamlaka husika za kisheria. Hatua zifuatazo zawaeza kukusaidia katika kupanga,kujiandaa na kuingoza biashara yako kwa ufanisi mkubwa zaidi: Andaa mwongozo wa biashara ( Business plan) Mwongozo huu utakusaidia  kukupa dira ya namna ya kuanza na kuendesha biashara yako kwa ufanisi. Tafuta msaada na mafunzo ya kibiashara Tumia fursa za bure za kujifunza  zinazopatikana mtandaoni au fursa za bei rahisi zinazotolewa katika makongamano ya ujasiriamali na uwekezaji hapa nchini. Chagua eneo sahihi la kuiweka biashara yako. Tafuta us

Mambo muhimu kuhusu mkopo - Sehemu ya 1

            Utangulizi  MKOPO ni kiwango cha fedha ambacho mtu hupewa na taasisi ya kifedha na kutakiwa kurudisha kiwango hicho kikiwa na riba kwa kipindi cha muda fulani. Mkopo unaweza  kuwa katika  mfumo wa bidhaa au kifaa lakini vitu hivyo  vyote hatimaye lazima thamani yake ipimwe na fedha,kwasababu  kazi kubwa ya fedha ni kupima thamani ya bidhaa au vifaa,mfano mtu anapochukua mkopo wa bidhaa zenye thamani ya Milioni kumi,tafsiri  yake ni kwamba umechukua mkopo wa Milioni kumi. Katika makala hii nitaeleza kuhusu mkopo kwa ujumla ingawa kwa sehemu kubwa nitaeleza juu ya mkopo wa fedha  unaotolewa na taasisi za za kifedha. Watu wamezoea kuwa mabenki ndiyo yanayo husika na utoaji wa mikopo tu lakini kiuhalisia kuna taasisi nyingi za kifedha zinazo husika na utoaji wa mikopo . Kulingana na sheria ya benki na taasisi za kifedha vyombo ambayo vinaruhusiwa na huduma ya utoaji mikopo ni benki ,saccos ,makampuni ya mikopo na mifuko ya hifadhi ya jamii. Tafiti zinaonyes

Mambo sita ya msingi kuhusu soko la bidhaa yako au huduma unayotoa

Sokoni ni eneo ambalo wauzaji wa bidhaa na wanunuzi wa bidhaa hukutana kubadilisha thamani vitu. Katika nyakati hizi soko la bidhaa linaweza kuwa ni kwa njia ya mtandao hivyo sio lazima mnunuzi na muuzaji wa bidhaa kukutana uso kwa uso. Kipindi hiki ni zama za sayansi na teknolojia ambazo zimetoa matumizi makubwa ya mtandao katika shughuli za mwanadamu hususani biashara hivyo kuna biashara nyingi zinafanyika kwenye mtandaoni (Online). Ninaamini wengi wetu tumeingia katika shughuli za ujaseriamali kwa dhumuni la kuongeza kipato hatimaye kuwa na maisha mazuri. Hivyo basi swala la soko katika biashara yako ni muhimu sana kwasababu bidhaa unazozalisha ni kwaajili ya kuuza na kupata faida.Katika biashara ya aina yoyote mzalishaji hana budi afahamu mambo kadhaa ya msingi kuhusu soko la bidhaa yake au huduma na kisha  kumsaidia kufanya maamuzi ya kumuwezesha kupata faida ya juu katika biashara anayoifanya. 1.Unahitaji kufanya utafiti wa kina juu ya soko la bidhaa z