Skip to main content

Kuongeza Thamani Katika Biashara

 Kuongeza thamani katika biashara ni kitu muhimu kwaajili ya ukuaji na mafanikio ya biashara yako kwa ujumla.

Thamani katika ulimwengu wa biashara inamaanisha ubora wa bidhaa/huduma kutoka na umuhimu wake ukilinganisha na pesa anayolipia mteja.

Biashara ambayo inatoa thamani kwa wateja wakati ni biashara ambayo itavutia wateja sana.

Unaweza kuongeza thamani katika biashara kwa kutumia njia mbalimbali lakini wewe kama mjasiriamali unahitaji kujua ni njia ipi ni sahihi katika biashara yako.

Njia za kuongeza thamani

Kuwajali wateja

Kuwajali wateja ni njia moja wapo ya kuongeza thamani katika biashara.

Wateja wanathamani na kupenda biashara ambayo inaridhisha zaidi ya mahitaji yao.

Hii inafanyika kwa kujifunza namna ya kuwajali wateja, kufanyia kazi malalamiko ya wateja, kutoa mrejesho wa wakati, kugusa hitaji la mteja wakati unamuhudumia.

Mara nyingi wateja wakijaliwa vizuri huwa wanawaambia watu wengine kuhusu ubora wa huduma na bidhaa zako. jambo ambalo huongeza mauzo na mapato katika biashara.

Kutoa huduma bora

Njia nyingine ya kuongeza thamani katika biashara yako ni kutoa huduma/bidhaa bora kwa wateja.

Wateja huwa wako tayari kulipia huduma/bidhaa ambazo zina ubora wa hali ya juu.

Unaweza kutumia malighafi zenye ubora kutengenezea bidhaa zako au kutumia watu wenye ujuzi kutengeneza bidhaa.

Ukitengeneza bidhaa zenye ubora itakusaidia kujitofautisha na wafanyabiashara wengine sokoni.

Kuboresha urahisi

Hii inaweza kufanyika kupitia huduma au biashara kupatikana kwa urahsi, kufungasha bidhaa vizuri na (faster delivery) kupeleka kwa wateja kwa wakati.

Wateja wanapoona unafanya delivery kwa wakati, umefunga bidhaa vizuri huamini hiyo bidhaa ina thamani.

Kumshauri Mteja 

Kabla ya mteja kununua bidhaa unamueleza manufaa ambayo atapata akinunua hiyo bidhaa.

Mteja akishanunua bidhaa unamshauri namna nzuri ya kutumia bidhaa au huduma ili apate manufaa zaidi.

Kumshauri kunaweza kuwa sambamba na matunzo ya hiyo bidhaa

Mfano Mteja amenunua simu unamueleza namna bora ya kutunza betri ya simu yake ni kuepuka kuchaji simu wakati anatumia.

Kuchaji simu wakati amepokea notification kuwa betri ni low na sio kuchaji tu simu wakati wowote.

Mwisho, mfanya biashara ambaye anathamini biashara yake wateja wake wataithamini hiyo biashara.

 


Comments

Popular posts from this blog

Hatua tisa za kuanzisha biashara.

Kuanzisha biashara kunahitaji kupanga mipango, kufanya maamuzi ya kifedha  na kutimiza  taratibu kadhaa za kisheria.  Wakati mwingine sio lazima kuzifanya  hatua zote kwa wakati mmoja lakini kadri biashara inavyozidi kuimarika basi ni lazima uzitimize hizo hatua muhimu. Kuna baadhi ya hatua ambazo ni lazima uzifanye mwanzoni kabisa mwa biashara yako, vinginevyo biashara yako itakufa ingali bado changa au itasimamishwa na mamlaka husika za kisheria. Hatua zifuatazo zawaeza kukusaidia katika kupanga,kujiandaa na kuingoza biashara yako kwa ufanisi mkubwa zaidi: Andaa mwongozo wa biashara ( Business plan) Mwongozo huu utakusaidia  kukupa dira ya namna ya kuanza na kuendesha biashara yako kwa ufanisi. Tafuta msaada na mafunzo ya kibiashara Tumia fursa za bure za kujifunza  zinazopatikana mtandaoni au fursa za bei rahisi zinazotolewa katika makongamano ya ujasiriamali na uwekezaji hapa nchini. Chagua eneo sahihi la kuiweka biashara yako. Tafuta us

Mambo muhimu kuhusu mkopo - Sehemu ya 1

            Utangulizi  MKOPO ni kiwango cha fedha ambacho mtu hupewa na taasisi ya kifedha na kutakiwa kurudisha kiwango hicho kikiwa na riba kwa kipindi cha muda fulani. Mkopo unaweza  kuwa katika  mfumo wa bidhaa au kifaa lakini vitu hivyo  vyote hatimaye lazima thamani yake ipimwe na fedha,kwasababu  kazi kubwa ya fedha ni kupima thamani ya bidhaa au vifaa,mfano mtu anapochukua mkopo wa bidhaa zenye thamani ya Milioni kumi,tafsiri  yake ni kwamba umechukua mkopo wa Milioni kumi. Katika makala hii nitaeleza kuhusu mkopo kwa ujumla ingawa kwa sehemu kubwa nitaeleza juu ya mkopo wa fedha  unaotolewa na taasisi za za kifedha. Watu wamezoea kuwa mabenki ndiyo yanayo husika na utoaji wa mikopo tu lakini kiuhalisia kuna taasisi nyingi za kifedha zinazo husika na utoaji wa mikopo . Kulingana na sheria ya benki na taasisi za kifedha vyombo ambayo vinaruhusiwa na huduma ya utoaji mikopo ni benki ,saccos ,makampuni ya mikopo na mifuko ya hifadhi ya jamii. Tafiti zinaonyes

Mambo sita ya msingi kuhusu soko la bidhaa yako au huduma unayotoa

Sokoni ni eneo ambalo wauzaji wa bidhaa na wanunuzi wa bidhaa hukutana kubadilisha thamani vitu. Katika nyakati hizi soko la bidhaa linaweza kuwa ni kwa njia ya mtandao hivyo sio lazima mnunuzi na muuzaji wa bidhaa kukutana uso kwa uso. Kipindi hiki ni zama za sayansi na teknolojia ambazo zimetoa matumizi makubwa ya mtandao katika shughuli za mwanadamu hususani biashara hivyo kuna biashara nyingi zinafanyika kwenye mtandaoni (Online). Ninaamini wengi wetu tumeingia katika shughuli za ujaseriamali kwa dhumuni la kuongeza kipato hatimaye kuwa na maisha mazuri. Hivyo basi swala la soko katika biashara yako ni muhimu sana kwasababu bidhaa unazozalisha ni kwaajili ya kuuza na kupata faida.Katika biashara ya aina yoyote mzalishaji hana budi afahamu mambo kadhaa ya msingi kuhusu soko la bidhaa yake au huduma na kisha  kumsaidia kufanya maamuzi ya kumuwezesha kupata faida ya juu katika biashara anayoifanya. 1.Unahitaji kufanya utafiti wa kina juu ya soko la bidhaa z