Skip to main content

Biashara Zenye Mtaji Mdogo

 Biashara zenye mtaji mdogo ni changamoto kuzianzisha lakini ni jambo linawezekana

Kuna njia nyingi za kuanza biashara ndogo au biashara ndogo na za kati (SMEs) hata kama una rasilimali chache.

Hapa kuna baadhi ya mawazo ya biashara zenye mtaji mdogo unazoweza kuzingatia nchini Tanzania.

Kuuza Nguo za Mitumba (Mitumba Business)

Unaweza kuanzisha biashara ya kuuza nguo za mitumba. 

Maendeleo ya teknolojia yamesadia upatikanaji wa mitandao ya kijamii kama Instagram, Facebook, Tiktok na mengine.

Mitandao yote hiyo inatoa fursa ya wewe kutangaza biashara yako na kufikia wateja wengi.

Biashara ya Chakula (Mamalishe/Babalishe)

Kutoa huduma za chakula kama vile kuuza vyakula vya asili, kufungua kibanda cha chakula, au kutoa huduma za catering.

Biashara ya Ukarimu (Guest House):

Kama una nyumba ya ziada au vyumba vichache, unaweza kuanzisha biashara ya nyumba za kulala wageni.

Huduma za Saluni na Urembo

Kutoa huduma za urembo kama vile kunyoa nywele, kupamba nywele, na huduma nyingine za uzuri.

Kuandaa Matukio (Event Planning):

Kama unaweza kupanga na kuandaa matukio, unaweza kuanzisha biashara ya kuandaa harusi, sherehe, au mikutano midogo.

Biashara ya Kilimo cha Mboga na Matunda

Kilimo kidogo cha mboga na matunda kinaweza kuanzishwa hata kwenye nafasi ndogo. Unaweza kuanza na mazao kama vile nyanya, pilipili, na mboga nyingine.

Biashara ya Vifaa vya Ujenzi:

Kuuza vifaa vya ujenzi au kutoa huduma za ujenzi kama vile ukarabati wa nyumba.

Hapa unaweza kutengeneza mtandao na mafundi ujenzi lakini pia kupatana na watu wenye maduka ya vifaa vya ujenzi pamoja na watu wenye  mahitaji ya vifaa vya ujenzi.

Fungua akaunti ya mitandao ya jamii kwa jina la biashara yako.

Weka bidhaa za ujenzi zinazopatikana kwenye maduka ya watu wa hardware kisha tangazo.

Usisahau kuwa na makubaliano rasmi na wenye maduka ikibainisha kiwango cha pesa utachapokea.

Faida kulinga na mauzo uliyofanya kwa mteja ambaye wewe ndio umempelekea dukani.

Huduma za Kusafisha (Cleaning Services):

Kutoa huduma za usafishaji kwa makampuni au nyumba binafsi.

Biashara ya Ushauri wa Kibiashara

Kama una ujuzi katika eneo fulani, unaweza kutoa huduma za ushauri wa biashara.

Hili ni eneo ambalo linahitaji uwe na ujuzi ili kuweza kuwahudumia wateja wako vizuri kulingana na mahitaji yao ya biashara.Biashara Mtandaoni

Kuanzisha biashara mtandaoni kama vile duka la mtandaoni, huduma za kuandika, au kutoa kozi mtandaoni.

Ni muhimu kufanya utafiti wa soko na kutengeneza mpango wa biashara kabla ya kuanza biashara yoyote.

Kumbuka kuwa umakini na ubunifu vinaweza kuchangia mafanikio ya biashara yako.

Comments

Popular posts from this blog

Hatua tisa za kuanzisha biashara.

Kuanzisha biashara kunahitaji kupanga mipango, kufanya maamuzi ya kifedha  na kutimiza  taratibu kadhaa za kisheria.  Wakati mwingine sio lazima kuzifanya  hatua zote kwa wakati mmoja lakini kadri biashara inavyozidi kuimarika basi ni lazima uzitimize hizo hatua muhimu. Kuna baadhi ya hatua ambazo ni lazima uzifanye mwanzoni kabisa mwa biashara yako, vinginevyo biashara yako itakufa ingali bado changa au itasimamishwa na mamlaka husika za kisheria. Hatua zifuatazo zawaeza kukusaidia katika kupanga,kujiandaa na kuingoza biashara yako kwa ufanisi mkubwa zaidi: Andaa mwongozo wa biashara ( Business plan) Mwongozo huu utakusaidia  kukupa dira ya namna ya kuanza na kuendesha biashara yako kwa ufanisi. Tafuta msaada na mafunzo ya kibiashara Tumia fursa za bure za kujifunza  zinazopatikana mtandaoni au fursa za bei rahisi zinazotolewa katika makongamano ya ujasiriamali na uwekezaji hapa nchini. Chagua eneo sahihi la kuiweka biashara yako. Tafuta us

Mambo muhimu kuhusu mkopo - Sehemu ya 1

            Utangulizi  MKOPO ni kiwango cha fedha ambacho mtu hupewa na taasisi ya kifedha na kutakiwa kurudisha kiwango hicho kikiwa na riba kwa kipindi cha muda fulani. Mkopo unaweza  kuwa katika  mfumo wa bidhaa au kifaa lakini vitu hivyo  vyote hatimaye lazima thamani yake ipimwe na fedha,kwasababu  kazi kubwa ya fedha ni kupima thamani ya bidhaa au vifaa,mfano mtu anapochukua mkopo wa bidhaa zenye thamani ya Milioni kumi,tafsiri  yake ni kwamba umechukua mkopo wa Milioni kumi. Katika makala hii nitaeleza kuhusu mkopo kwa ujumla ingawa kwa sehemu kubwa nitaeleza juu ya mkopo wa fedha  unaotolewa na taasisi za za kifedha. Watu wamezoea kuwa mabenki ndiyo yanayo husika na utoaji wa mikopo tu lakini kiuhalisia kuna taasisi nyingi za kifedha zinazo husika na utoaji wa mikopo . Kulingana na sheria ya benki na taasisi za kifedha vyombo ambayo vinaruhusiwa na huduma ya utoaji mikopo ni benki ,saccos ,makampuni ya mikopo na mifuko ya hifadhi ya jamii. Tafiti zinaonyes

Mambo sita ya msingi kuhusu soko la bidhaa yako au huduma unayotoa

Sokoni ni eneo ambalo wauzaji wa bidhaa na wanunuzi wa bidhaa hukutana kubadilisha thamani vitu. Katika nyakati hizi soko la bidhaa linaweza kuwa ni kwa njia ya mtandao hivyo sio lazima mnunuzi na muuzaji wa bidhaa kukutana uso kwa uso. Kipindi hiki ni zama za sayansi na teknolojia ambazo zimetoa matumizi makubwa ya mtandao katika shughuli za mwanadamu hususani biashara hivyo kuna biashara nyingi zinafanyika kwenye mtandaoni (Online). Ninaamini wengi wetu tumeingia katika shughuli za ujaseriamali kwa dhumuni la kuongeza kipato hatimaye kuwa na maisha mazuri. Hivyo basi swala la soko katika biashara yako ni muhimu sana kwasababu bidhaa unazozalisha ni kwaajili ya kuuza na kupata faida.Katika biashara ya aina yoyote mzalishaji hana budi afahamu mambo kadhaa ya msingi kuhusu soko la bidhaa yake au huduma na kisha  kumsaidia kufanya maamuzi ya kumuwezesha kupata faida ya juu katika biashara anayoifanya. 1.Unahitaji kufanya utafiti wa kina juu ya soko la bidhaa z