Skip to main content

Posts

Showing posts from July, 2016

Mambo muhimu katika biashara

Katika kila taaluma kwenye maisha ya mwanadamu kuna taratibu zake au kuna kanuni fulani ambazo zinasaidia kutoa mwongozo kwa kila anayetaka kufanya jambo hilo ili aweze kufanya katika ubora unao kubalika.  Vivyo hivyo katika biashara  kuna mambo muhimu ambayo mjasiriamali  anapaswa kuzingatia ili aweze kufanya kazi yake katika viwango vilivyo tukuka.  Una zalisha bidhaa zako kwaajili ya nani ? hili ni swali la msingi ambalo mfanyabiashara yoyote anapaswa kujiuliza kabla ya kuanza kutengeneza bidhaa zake. Kuna utofauti mkubwa kati ya utengenezaji wa bidhaa kulingana umri, utamaduni wa watu fulani ,taaluma ya watu fulani, mila na desturi za watu fulani na wakati mwingine pia kulingana na hali ya kijiografia ya eneo husika itakuwa jambo la ajabu kama mjasiriamali ataamua kutengeneza makoti mazito na masweta wakati anategemea wateja wake wanapatikana katika ukanda wa joto. Ni vyema mfanyabiashara  akajua vyema aina ya kundi katika jamii ambalo amekusudia kuliuzia baid

Piga hatua katika biashara yako

Hatua ni umbali kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine au kutoka kiwango kimoja kwenda kiwango kingine. Mtu ambaye hapigi hatua katika biashara yake ni mtu ambaye yuko kwenye kiwango kimoja tu cha biashara kwa kipindi cha muda mrefu. Mtu anapokuwa anapanda ngazi au kushuka ni lazima apige hatua moja ikifuatiwa na hatua nyingine na kadri atakavyokuwa akiendelea ndivyo atakuwa akiikaribia hatima yake au mahali alipotakiwa kufika. Hatua kwenye biashara ni mfano wa ngazi hivyo unapaswa kupiga  hatua moja kwenda nyingine ili uweze kufikia hatima yako. Katika biashara kuna watu aina tatu. (i) Watu ambao hupiga hatua kwenda mbele mfano mwaka jana alikuwa na mtaji wenye thamani ya shilling 1,000,000 mwaka huu ameongeza mtaji wake kufikia thamani ya shilingi 1,500,000. (ii) Watu ambao hawapigi hatua kabisa mfano mwaka jana alikuwa na mtaji wenye thamani ya 500,000 na mwaka huu thamani ya mtaji wake ni shilingi 500,000. (iii) Watu ambao wanapiga hatua kurudi nyu