Skip to main content

Posts

Showing posts from August, 2019

USIMAMIZI WA FEDHA KATIKA BIASHARA YAKO

                                               SEHEMU YA KWANZA UTANGULIZI  Moja kati ya elimu muhimu sana kwa kila mjasiariamali ni elimu kuhusu usimamizi wa fedha, elimu ya usimamizi wa fedha ndiyo itakayo msaidia mjasiriamali kuwa na uendelevu  (Stability( katika biashara yake kwasababu suala sio kuwa na biashara tu bali ni kuwa na biashara yenye kuendelea. Usimamizi wa fedha ni kitendo cha kuweka mipango na kudhibiti shughuli zote zinazo husu masuala ya fedha katika biashara, kampuni au taasisi fulani.  Kwanini unapaswa kujifunza usimamizi wa fedha katika biashara yako . 1. Unapaswa kujifunza usimamizi wa fedha kwasababu ili uwezekujua ni njia ipi inaweza kukusaidia kukuza mtaji wako kama lakini katika hatua ya awali ni vema ukalifahamu hili kwasababu itakusaidia kujua mahitaji yako ya mtaji kulinga na biashara unayokusudia kuanzisha.   i) Mkopo  ii) Kuweka fedha zako mwenyewe iii) Mkopo na fedha zako mwenyewe 2. Unapaswa kujua usimamizi wa fedh

SAFARI YA UJASIRIAMALI

Safari ya ujasiriamali ni safari kama zilivyosafari nyingine katika maisha ya mwanadamu Kuna mambo ya muhimu unapaswa kufahamu kama mjasiamali ili uweze kusafiri vizuri katika shughuli zako 1. Safari yako ni lazima iwe na hatima lakini ni lazima uone hatima ya safari yako mwanzoni. 2. Safari yako ni ya pekee, namna utakavyo safiri ni tofauti na wajasiriamali wengine. 3. Umbali wa safari yako ni tofauti na safari za watu wengine. 4. Katika safari kuna changamoto mbalimbali ambazo huna budi kukabiliana nazo ilikufikia hatima yako. 5. Katika safari yako ni lazima kufuata sheria za mamlaka husika ilikuepuka usumbufu na adhabu zinazoweza kuzuia kufika au kukuchelesha kufikia hatima yako. Itaendelea Imeandikwa na James Albert Whatsapp namba +255717162510 Barua pepe jamesalbert157@gmail.com