Skip to main content

Posts

Showing posts from September, 2023

Kuongeza Thamani Katika Biashara

 Kuongeza thamani katika biashara ni kitu muhimu kwaajili ya ukuaji na mafanikio ya biashara yako kwa ujumla. Thamani katika ulimwengu wa biashara inamaanisha ubora wa bidhaa/huduma kutoka na umuhimu wake ukilinganisha na pesa anayolipia mteja. Biashara ambayo inatoa thamani kwa wateja wakati ni biashara ambayo itavutia wateja sana. Unaweza kuongeza thamani katika biashara kwa kutumia njia mbalimbali lakini wewe kama mjasiriamali unahitaji kujua ni njia ipi ni sahihi katika biashara yako. Njia za kuongeza thamani Kuwajali wateja Kuwajali wateja ni njia moja wapo ya kuongeza thamani katika biashara. Wateja wanathamani na kupenda biashara ambayo inaridhisha zaidi ya mahitaji yao. Hii inafanyika kwa kujifunza namna ya kuwajali wateja, kufanyia kazi malalamiko ya wateja, kutoa mrejesho wa wakati, kugusa hitaji la mteja wakati unamuhudumia. Mara nyingi wateja wakijaliwa vizuri huwa wanawaambia watu wengine kuhusu ubora wa huduma na bidhaa zako. jambo ambalo huongeza mauzo na mapato katika

Masoko Ya Mitandao Ya Kijamii.

  Masoko ya mitandao ya kijamii ni mchakato wa kutengeneza na kushirikisha maudhui  watu yenye lengo la kutangaza huduma/bidhaa yako kupitia mitandao ya kijamii. Baadhi ya mitandao ya kijamii ni kama Facebook, Instagram, Twitter, LinkedIn, Threads na Truth Socia Media. Lengo la masoko ya mitandao ya kijamii ni kuwajengea wateja uelewa. Kuhusu huduma/bidhaa zako, kuongeza watembeleaji wa tovuti ya biashara na kuongeza mauzo kwa ujumla. Masoko ya mitandao ya kijamii yanahitaji ufahamu wa hali ya juu kufikia wateja ambao umewakusudia. Mfano wateja kusudiwa wanaweza kuwa wanawake miaka 22-35, wanaume umri wa miaka 25-35, watu wasiokua na ajira nk. Kimsingi aina ya wateja uliowakusudia ndio inaamua aina ya maudhui ambayo utatakiwa kuandika kwenye mitandao ya kijamii. Ifahamike matangazo ya biashara ni kwaajili ya wateja na sio kwaajili yako mwenyewe hivyo andika kulingana na aina ya wateja wako. Kwanini Ni Muhimu Kutangaza Biashara Yako Kupitia Masoko ya Mitandao Ya Kijamii.  1.Inaongeza

Jinsi Ya Kuanzisha Blog Yenye Kukuingizia Pesa.

 Kupitia blog unaweza kuijingiza kipato kizuri sana ikiwa kazi hii utaifanya kwa ubora wa hali ya juu. Kuanzisha blog yenye kuingiza kipato mtandaoni linaweza kuwa jambo geni na la kushangaza kwa baadhi ya watu kwasababu huenda hawajawahi kujua namna blog inavyoweza kuingiza kipato. Ukweli ni kwamba nimefanya blogging kwa kipindi cha muda wa miaka 7 lakini nilipoanza mwaka wa 8 ndio nilianza kutafuta namna ya kuingizia kipato. mtandaoni Baada ya kujifunza namna nilivyoweza kujifunza kuingiza kipato kupitia blog mtandaoni nimeona ni vyema nikushirikishe na wewe. Mentor wangu kwenye Blog Ally Msangi aliwahi kusema “Blogging ni biashara ambayo ukifanya serious inalipa vizuri sana” Hii ni moja ya kauli ambayo ilinifanya kugeuza mtazamo wangu kwa kiasi kikubwa kwenye masuala ya Blogging. Je Blogging ni  nini ? Blogging ni kitendo cha kutengeneza maudhui na kuyachapisha katika mtandao wa intaneti. Kuanza biashara ya Blogging inaweza kuwa jambo gumu lakini ukiwa na ushauri wa kitalamu ni j

Mambo Muhimu Kuhusu Soko

 Mambo muhimu kuhusu mikopo kabla ya kuchukua mkopo katika taasisi za kifedha. Zifuatazo ni dondoo muhimu kuhusu mikopo. 1.Dhumuni lako ni nini Ni vizuri ukajihoji binafsi unachukua mkopo kwaajili ya kufanyianin?. Jambo la ajabu na la kusikitisha endapo utachukua mkopo kwa ajili ya matumizi ya kawaida mfano kununulia nguo,chakula na kadhalika. Chukua mkopo kwa dhumuni la kufanyia biashara yaani chukua fedha ili uzalishe fedha. 2 . Je ni kiwango gani cha fedha kinaweza kukidhi haja ya biashara yako au thamani unayohitaji kununua Unahitaji kiwango gani cha fedha  unapokwenda katika taasisi za kifedha kama benki na saccos moja kati ya swali muhimu ambalo utaulizwa ni kiwango gani cha fedha unahitaji?. Awali, kuwa na mpango kazi(Business Plan) wa biashara yako ambayo imebeba mchanganuo wa biashara yako kwa kina. Mpango kazi wenyewe uwe na uwezo wa kujibu maswali mengi ambayo taasisi za kifedha zitakuuliza. 3.Je unathamani ambayo unaweza kuweka rehani kulinda huo mkopo endapo utashindwa kul

Nichi Ya Soko

 Nichi ya soko kwaajili ya biashara ni suala la msingi kwaajili ya ustawi wa biashara yako .  Kwa maneno mengine ni eneo maalamu la soko ambalo linakua na bidhaa/huduma maalumu. Ina maanisha  kipande cha soko ambacho kina mahitaji tofauti, sifa na machaguo tofauti ya wateja. Kipande hiki cha soko kinaweza kubainishwa kwa kutumia vigezo mbalimbali. Mfano tabia za watumia huduma, mtindo wa maisha wa watumia huduma, eneo ambalo watumia huduma hupatikana Katika soko kubwa ndani yake kuna masoko madogomadogo mfano soko la viatu, nguo, matunda, vifaa vya umeme na masoko mengine. Mfano biashara ya suruali za jinsi hii ni nichi kamili. Nichi hii inaelezea bayana watumiaji kwa asilimia kubwa watakuwa ni vijana wenye umri kati ya miaka 18-35 kwasababu umri huo ndio kuna vijana. Pia ni kundi ambalo linabadilika  kwa urahisi kulingana na mtindo na wakati. Mfanyabiashara anaye chagua nichi ya suruali za  jeans ni lazima awe ni mtu ambaye anafuatilia matulio ya jeans mpya kulinga na mtindo mpya kil