ANGALIA UNAPENDA NINI KISHA KIGEUZE KUWA BIDHAA AU HUDUMA. Kuna idadi kubwa ya watu ambao wamepata mawazo ya kuanzisha biashara kupitia njia hii na hatimaye kujitengenezea kipato kizuri. Kila mwanadamu kuna jambo fulani au kitu fulani ambacho yeye anapenda kufanya hivyo ni vyema ukajichunguza unapenda nini na hatimaye kugeuza hicho unachopenda kuwa bidhaa au huduma. Mfano I Kama wewe unapenda shughuli za kilimo unaweza kuanzisha shughuli za kilimo biashara (Agribusiness) ukijikita katika uzalishaji wa mazao ya biashara, pia waweza kuanzisha kiwanda cha usindikaji wa mazao ya kilimo ili kuongeza thamani na kisha kijitengenezea kipato kizuri kabisa. Mfano II Kama wewe unapenda maswala ya mitindo na urembo waweza kuanzisha kampuni itakayokuwa inashughulika na utengenezaji wa nguo ,vipodozi usambazi marashi ,mafuta ya kujipaka na bidhaa nyingine zinazohusika na mitindo na urembo.Unaweza kuanzisha saluni za kiume na za kike ilikuweza kufanya jambo unalolipenda
Jukwa maalumu kwaaji ya kujifunza masuala mbalimbali kuhusu biashara na ujasiriamali