Skip to main content

Posts

Showing posts from September, 2021

MALEZI YA BIASHARA

                                                        UTANGULIZI Suala la malezi ni suala muhimu sana kwenye kila eneo la maisha hususani eneo la biashara ambalo makala hii imejikitaza kuelezea.  Mlezi wa biashara ni mtu ambaye mjasiriamali anamchagua makusudi kwa lengo la kupata malezi katika masuala ya kibiashara.  Uamuzi wa kupata mlezi wa biashara unapaswa kwa umakini mkubwa ili kuweka mazingira salama  yatakayowezesha ukuaji na maendeleo ya biashara yako.  Hakuna kanuni maalumu ambayo kila mfanyabiashara ameipitia ilikupata mlezi wa biashara lakini kuna dondoo muhimu ambazo ni vizuri kuzifahamu ili kuweza kupata msingi wa kufanya maamuzi yenye tija.  Kwanini unahitaji kuwa na mlezi katika biashara? i) Kuepuka makosa ambayo yanaweza kuepukika ii) Kuwa na mshauri na mwangalizi iii) Kuongeza kiwango cha uwajikabaji iv) Kuongeza mtandao wa kibiashara v) Kuwa na mtu wa kumueleza changamoto ili kupunguza msongo wa mawazo  Kama mfanya biashara na mjasiriamali ni vizuri ukawa na mlezi w

NGUZO YA UBUNIFU

                                                        SEHEMU YA I  Moja ya kitu ambacho kinaweza kumpa mjasiriamali nguvu ya kuteka soko la bidhaa au huduma fulani ni Ubunifu. Kimsingi huduma huduma na bidhaa nyingi tayari zimekuwepo sokoni kwa kipindi cha miaka kadha na ni nadra sana kuona mjasiriamali anakuja na bidhaa/huduma ambayo haijawahi kuwepo sokoni.  Ubunifu ni hali au uwezo mpya wa kutoa huduma tofauti yenye ubora wa juu kuliko huduma iliyokuwepo sokoni au kuja na namna mpya ya kutoa huduma fulani ambayo ni tofauti wa wauzaji wengine wa bidhaa/huduma hiyo.  Unaweza kukuta katika eneo moja kuna wauzaji wa nafaka wengine lakini kuna muuzaji mmoja ambaye ndiye mwenye wateja wengi kuliko wengine na ukichunguza utandua kuna kitu huyo mjasiriamali anacho ambacho wengine hawana kabisa kitu hicho. Inaweza kuwa ni kauli nzuri, namna nzuri ya kufunga mzigo (packagging), bei nafuu, usafi wa eneo, kutoa ziada ya huduma mfano unaweza kukuta mjasiriamali anauza mahindi na huduma ya zia