Skip to main content

Mambo muhimu katika biashara





Katika kila taaluma kwenye maisha ya mwanadamu kuna taratibu zake au kuna kanuni fulani ambazo zinasaidia kutoa mwongozo kwa kila anayetaka kufanya jambo hilo ili aweze kufanya katika ubora unao kubalika. 


Vivyo hivyo katika biashara  kuna mambo muhimu ambayo mjasiriamali  anapaswa kuzingatia ili aweze kufanya kazi yake katika viwango vilivyo tukuka. 

Una zalisha bidhaa zako kwaajili ya nani ? hili ni swali la msingi ambalo mfanyabiashara yoyote anapaswa kujiuliza kabla ya kuanza kutengeneza bidhaa zake. Kuna utofauti mkubwa kati ya utengenezaji wa bidhaa kulingana umri, utamaduni wa watu fulani ,taaluma ya watu fulani, mila na desturi za watu fulani na wakati mwingine pia kulingana na hali ya kijiografia ya eneo husika itakuwa jambo la ajabu kama mjasiriamali ataamua kutengeneza makoti mazito na masweta wakati anategemea wateja wake wanapatikana katika ukanda wa joto. Ni vyema mfanyabiashara  akajua vyema aina ya kundi katika jamii ambalo amekusudia kuliuzia baidhaa zake. 


Je upatikanaji wa mali ghafi ukoje ? mali ghafi ni vitu vyote ambavyo vinasaidia katika utengenezaji wa bidhaa, mfano kama wewe una mghahawa basi mali ghafi yako ni chumvi, sukari, mchele nk. Kujua upatikanaji wa mali ghafi kutakusaidia kujua ni wapi ufungue kituo chako cha biashara, itakusaidia kujua upange bei gani kulingana na gharama ya upatikanaji wa mali ghafi.

Je bidhaa yako ni ya msimu au la ? kila mfanyabishara anapaswa kujua aina ya bidhaa anayozalisha je inasoko la kudumu au ni bidhaa ya msimu tu. Kupitia kujua aina ya soko la bidhaa zake itamsaidia kujua ni kiwango gani anapaswa kuzalisha au kununua na kisha kwenda kuuza kwenye soko husika.

Je washindani wako ni kina nani ? washindani wako ni makampuni au watu wanaozalisha bidhaa zinazofanana na za kwako. Ukijua washindani wako itakusaidia kuzalisha bidhaa zenye ubora na utofauti ukilinganisha na wao hivyo utakuwa na uhakika wa soko la bidhaa zako.


Je utahitaji kufanya matangazo ya biashara yako ? Ulimwengu wa sasa ni ulimwengu wa kidigitali, na kumekuwa na matumizi makubwa ya teknolojia ya habari na wasaliliano hivyo ni vyema ukajua njia sahihi ya kutangaza biashara yako. Kuna utofauti mkubwa wa kutangaza biashara kwenye redio, televisheni, majarida, vipeperushi, mabango na hata katika tovuti. Mfano, matangazo ya kwenye  mitandao ya kijamii yanapaswa kuwa na ujumbe wa moja kwa moja na mvuto wa picha wa hali ya juu kiasi kwamba  tangazo hilo litakamata akili ya anayeperuzi kwa urahisi ili aendelee kusoma na kuliangalia tangazo hilo. 


Uzuri wa kazi yoyote katika biashara unategemea na umakini wa mfanyabishara katika kuzingatia mambo muhimu yenye kutoa mwongozo wa kibiashara. Ni hekima kwa mfanyabiashara kujifunza mambo hayo muhimu kabla ya kuingia katika biashara. Swala la msingi  zaidi analopaswa kufahamu mfanyabiashara ni kwamba kuna mambo mengi katika biashara hivyo anaweza kujifunza moja baada ya jingine huku akiweka katika matendo kile anachojifunza. Mfano anaweza kujifunza maswala ya Soko, Usimamizi wa biashara, Usimamizi wa miradi nk.

Itaendelea.

By
James Albert.

Comments

Popular posts from this blog

Hatua tisa za kuanzisha biashara.

Kuanzisha biashara kunahitaji kupanga mipango, kufanya maamuzi ya kifedha  na kutimiza  taratibu kadhaa za kisheria.  Wakati mwingine sio lazima kuzifanya  hatua zote kwa wakati mmoja lakini kadri biashara inavyozidi kuimarika basi ni lazima uzitimize hizo hatua muhimu. Kuna baadhi ya hatua ambazo ni lazima uzifanye mwanzoni kabisa mwa biashara yako, vinginevyo biashara yako itakufa ingali bado changa au itasimamishwa na mamlaka husika za kisheria. Hatua zifuatazo zawaeza kukusaidia katika kupanga,kujiandaa na kuingoza biashara yako kwa ufanisi mkubwa zaidi: Andaa mwongozo wa biashara ( Business plan) Mwongozo huu utakusaidia  kukupa dira ya namna ya kuanza na kuendesha biashara yako kwa ufanisi. Tafuta msaada na mafunzo ya kibiashara Tumia fursa za bure za kujifunza  zinazopatikana mtandaoni au fursa za bei rahisi zinazotolewa katika makongamano ya ujasiriamali na uwekezaji hapa nchini. Chagua eneo sahihi la kuiweka biashara yako. Tafuta us

Mambo muhimu kuhusu mkopo - Sehemu ya 1

            Utangulizi  MKOPO ni kiwango cha fedha ambacho mtu hupewa na taasisi ya kifedha na kutakiwa kurudisha kiwango hicho kikiwa na riba kwa kipindi cha muda fulani. Mkopo unaweza  kuwa katika  mfumo wa bidhaa au kifaa lakini vitu hivyo  vyote hatimaye lazima thamani yake ipimwe na fedha,kwasababu  kazi kubwa ya fedha ni kupima thamani ya bidhaa au vifaa,mfano mtu anapochukua mkopo wa bidhaa zenye thamani ya Milioni kumi,tafsiri  yake ni kwamba umechukua mkopo wa Milioni kumi. Katika makala hii nitaeleza kuhusu mkopo kwa ujumla ingawa kwa sehemu kubwa nitaeleza juu ya mkopo wa fedha  unaotolewa na taasisi za za kifedha. Watu wamezoea kuwa mabenki ndiyo yanayo husika na utoaji wa mikopo tu lakini kiuhalisia kuna taasisi nyingi za kifedha zinazo husika na utoaji wa mikopo . Kulingana na sheria ya benki na taasisi za kifedha vyombo ambayo vinaruhusiwa na huduma ya utoaji mikopo ni benki ,saccos ,makampuni ya mikopo na mifuko ya hifadhi ya jamii. Tafiti zinaonyes

Mambo sita ya msingi kuhusu soko la bidhaa yako au huduma unayotoa

Sokoni ni eneo ambalo wauzaji wa bidhaa na wanunuzi wa bidhaa hukutana kubadilisha thamani vitu. Katika nyakati hizi soko la bidhaa linaweza kuwa ni kwa njia ya mtandao hivyo sio lazima mnunuzi na muuzaji wa bidhaa kukutana uso kwa uso. Kipindi hiki ni zama za sayansi na teknolojia ambazo zimetoa matumizi makubwa ya mtandao katika shughuli za mwanadamu hususani biashara hivyo kuna biashara nyingi zinafanyika kwenye mtandaoni (Online). Ninaamini wengi wetu tumeingia katika shughuli za ujaseriamali kwa dhumuni la kuongeza kipato hatimaye kuwa na maisha mazuri. Hivyo basi swala la soko katika biashara yako ni muhimu sana kwasababu bidhaa unazozalisha ni kwaajili ya kuuza na kupata faida.Katika biashara ya aina yoyote mzalishaji hana budi afahamu mambo kadhaa ya msingi kuhusu soko la bidhaa yake au huduma na kisha  kumsaidia kufanya maamuzi ya kumuwezesha kupata faida ya juu katika biashara anayoifanya. 1.Unahitaji kufanya utafiti wa kina juu ya soko la bidhaa z