Skip to main content

NGUZO YA UBUNIFU

                                                       SEHEMU YA I 



Moja ya kitu ambacho kinaweza kumpa mjasiriamali nguvu ya kuteka soko la bidhaa au huduma fulani ni Ubunifu. Kimsingi huduma huduma na bidhaa nyingi tayari zimekuwepo sokoni kwa kipindi cha miaka kadha na ni nadra sana kuona mjasiriamali anakuja na bidhaa/huduma ambayo haijawahi kuwepo sokoni. 

Ubunifu ni hali au uwezo mpya wa kutoa huduma tofauti yenye ubora wa juu kuliko huduma iliyokuwepo sokoni au kuja na namna mpya ya kutoa huduma fulani ambayo ni tofauti wa wauzaji wengine wa bidhaa/huduma hiyo. 

Unaweza kukuta katika eneo moja kuna wauzaji wa nafaka wengine lakini kuna muuzaji mmoja ambaye ndiye mwenye wateja wengi kuliko wengine na ukichunguza utandua kuna kitu huyo mjasiriamali anacho ambacho wengine hawana kabisa kitu hicho. Inaweza kuwa ni kauli nzuri, namna nzuri ya kufunga mzigo (packagging), bei nafuu, usafi wa eneo, kutoa ziada ya huduma mfano unaweza kukuta mjasiriamali anauza mahindi na huduma ya ziada ni mteja kubebewa mzigo au kupewa mfuko wa kubebea bure. 


KUNA VITU VYA MUHIMU VINAVYOMUWEZESHA MJASIRIMALI KUWA MBUNIFU

1. KUWA NA UEKEKEO THABITI

Ni muhimu sana mjasirimali kujua anahitaji kufanya nini katika biashara yake kabla hata ya kuanza hiyo biashara ili aweze kujua anapaswa kuwekeza kwenye nini, afanye biashara yake kwenye eneo gani, anampango wa kuwa na wateja wa aina gani, anahitaji kuuza huduma/bidhaa gani na mengine mengi. Kuwa na uelekeo thabiti inamsaidia mjasirimali kuwa na msingi mzuri wa kufanya maamuzi yenye tija na kuleta matokeo chanya katika biashara yake. 


2. KUTAFUTA MBADA WA HUDUMA/BIDHAA

Katika maisha yetu kuna biashara mbalimbali ambazo tayari zipo ili mjasirimali aweza kuwa na huduma bora anapswa kufanya uchunguzi wa bidhaa zilizopo zinaupungufu gani au kuna ombwe(gap) kati ya matarajio ya wateja na huduma inayotoletwa baada ya kubaini huo upungufu ni hekima kuja na biashara ambayo itakuwa na uwezo wa kutoa huduma bora na kwa namna ya kipekee ukilinganisha wa na huduma za wajasiriamali wengine waliopo sokoni. 

Itaendelea Sehemu ya II 

Imeandaliwa na James Albert 

Namba ya whatsapp 0717165210

Barua pepe jamesalbert157@gmail.com 


Comments

Popular posts from this blog

Hatua tisa za kuanzisha biashara.

Kuanzisha biashara kunahitaji kupanga mipango, kufanya maamuzi ya kifedha  na kutimiza  taratibu kadhaa za kisheria.  Wakati mwingine sio lazima kuzifanya  hatua zote kwa wakati mmoja lakini kadri biashara inavyozidi kuimarika basi ni lazima uzitimize hizo hatua muhimu. Kuna baadhi ya hatua ambazo ni lazima uzifanye mwanzoni kabisa mwa biashara yako, vinginevyo biashara yako itakufa ingali bado changa au itasimamishwa na mamlaka husika za kisheria. Hatua zifuatazo zawaeza kukusaidia katika kupanga,kujiandaa na kuingoza biashara yako kwa ufanisi mkubwa zaidi: Andaa mwongozo wa biashara ( Business plan) Mwongozo huu utakusaidia  kukupa dira ya namna ya kuanza na kuendesha biashara yako kwa ufanisi. Tafuta msaada na mafunzo ya kibiashara Tumia fursa za bure za kujifunza  zinazopatikana mtandaoni au fursa za bei rahisi zinazotolewa katika makongamano ya ujasiriamali na uwekezaji hapa nchini. Chagua eneo sahihi la kuiweka biashara yako. Tafuta us

Mambo muhimu kuhusu mkopo - Sehemu ya 1

            Utangulizi  MKOPO ni kiwango cha fedha ambacho mtu hupewa na taasisi ya kifedha na kutakiwa kurudisha kiwango hicho kikiwa na riba kwa kipindi cha muda fulani. Mkopo unaweza  kuwa katika  mfumo wa bidhaa au kifaa lakini vitu hivyo  vyote hatimaye lazima thamani yake ipimwe na fedha,kwasababu  kazi kubwa ya fedha ni kupima thamani ya bidhaa au vifaa,mfano mtu anapochukua mkopo wa bidhaa zenye thamani ya Milioni kumi,tafsiri  yake ni kwamba umechukua mkopo wa Milioni kumi. Katika makala hii nitaeleza kuhusu mkopo kwa ujumla ingawa kwa sehemu kubwa nitaeleza juu ya mkopo wa fedha  unaotolewa na taasisi za za kifedha. Watu wamezoea kuwa mabenki ndiyo yanayo husika na utoaji wa mikopo tu lakini kiuhalisia kuna taasisi nyingi za kifedha zinazo husika na utoaji wa mikopo . Kulingana na sheria ya benki na taasisi za kifedha vyombo ambayo vinaruhusiwa na huduma ya utoaji mikopo ni benki ,saccos ,makampuni ya mikopo na mifuko ya hifadhi ya jamii. Tafiti zinaonyes

Mambo sita ya msingi kuhusu soko la bidhaa yako au huduma unayotoa

Sokoni ni eneo ambalo wauzaji wa bidhaa na wanunuzi wa bidhaa hukutana kubadilisha thamani vitu. Katika nyakati hizi soko la bidhaa linaweza kuwa ni kwa njia ya mtandao hivyo sio lazima mnunuzi na muuzaji wa bidhaa kukutana uso kwa uso. Kipindi hiki ni zama za sayansi na teknolojia ambazo zimetoa matumizi makubwa ya mtandao katika shughuli za mwanadamu hususani biashara hivyo kuna biashara nyingi zinafanyika kwenye mtandaoni (Online). Ninaamini wengi wetu tumeingia katika shughuli za ujaseriamali kwa dhumuni la kuongeza kipato hatimaye kuwa na maisha mazuri. Hivyo basi swala la soko katika biashara yako ni muhimu sana kwasababu bidhaa unazozalisha ni kwaajili ya kuuza na kupata faida.Katika biashara ya aina yoyote mzalishaji hana budi afahamu mambo kadhaa ya msingi kuhusu soko la bidhaa yake au huduma na kisha  kumsaidia kufanya maamuzi ya kumuwezesha kupata faida ya juu katika biashara anayoifanya. 1.Unahitaji kufanya utafiti wa kina juu ya soko la bidhaa z