UTANGULIZI
Suala la malezi ni suala muhimu sana kwenye kila eneo la maisha hususani eneo la biashara ambalo makala hii imejikitaza kuelezea.
Mlezi wa biashara ni mtu ambaye mjasiriamali anamchagua makusudi kwa lengo la kupata malezi katika masuala ya kibiashara.
Uamuzi wa kupata mlezi wa biashara unapaswa kwa umakini mkubwa ili kuweka mazingira salama yatakayowezesha ukuaji na maendeleo ya biashara yako.
Hakuna kanuni maalumu ambayo kila mfanyabiashara ameipitia ilikupata mlezi wa biashara lakini kuna dondoo muhimu ambazo ni vizuri kuzifahamu ili kuweza kupata msingi wa kufanya maamuzi yenye tija.
Kwanini unahitaji kuwa na mlezi katika biashara?
i) Kuepuka makosa ambayo yanaweza kuepukika
ii) Kuwa na mshauri na mwangalizi
iii) Kuongeza kiwango cha uwajikabaji
iv) Kuongeza mtandao wa kibiashara
v) Kuwa na mtu wa kumueleza changamoto ili kupunguza msongo wa mawazo
Kama mfanya biashara na mjasiriamali ni vizuri ukawa na mlezi wako katika masuala ya biashara yako.
Zifuatazo ni dondoo muhimu katika kufanya maamuzi wa mlezi wa biashara
i) Mwenye maono
ii) Mwenye uzoefu katika biashara
iii) Mwenye uongozi bora katika biashara yake
iv) Mwenye mtazamo chanya na imani na wewe
Imeandaliwa na James Albert
Namba ya whatsapp 0717162510
Barua pepe jamesalbert157@gmail.com
Comments
Post a Comment