Skip to main content

Miundombinu ya uwekezaji - Part 2

Tunaendelea na Ujenzi wa Miundombinu ya uwekezaji:
Ili kujua ni aina gani ya miundombinu na yenye kiwango gani unatakiwa kuijenga ni lazima kwanza ujue ni uwekezaji wa ukubwa gani unaouhitaji hapo baadaye na ni aina gani ya sekta unayotaka kuwekeza, kama ilivyo kwa ujenzi wa majengo makubwa msingi ndio unao amua urefu na ukubwa wa jengo kadhalika katika uwekezaji miundombinu unayoiandaa tangu mwanzo ndio inayoamua ukubwa wa miradi unayoikusudia.
Jana nilipata nafasi ya kuitazama vizuri treni iliyokuwa ikipita umbali kama mita tatu hivi toka nilipokuwa nikajuliza maswali kadhaa
1. Kipi kilitangulia kati ya ujenzi wa Reli na ununuzi wa Treni na behewa zake ?

2. Kipi kinamwongoza mwenzie (amua mwelekeo) Je, ni treni ? au reli ?
3. Kipi kinaamua ukubwa na uzito wa mzigo unaobebwa je ni treni ama reli ? kama ingekuwa ni treni kuna ulazima gani wa Serikali yetu leo kujenga reli mpya kwa kiwango cha "Standard gauge " ?
Kwa maswali hayo nilijiridhisha kwamba miundombinu ya uwekezaji ni jambo la msingi kabla ya uwekezaji wowote ule, iko mifano mingi kwa wale wanaofuatilia watakua wanafahamu sababu kubwa iliyosababisha mradi wa boti ya Dar- Bagamoyo kushindwa kufanyakazi, kwa nini wakulima wanaandaa mashamba kwanza kabla ya kupanda, kwanini wanaangalia msimu wa kupanda jibu rahisi ni kuhakikisha miundombinu yote ya msingi iko sawa.
Swali ni je, katika mradi/miradi unayoianzisha sasa umeiwekea miundombinu mahususi inayoiwezesha kufika huko unakotaka ifike na kwa kiwango ulicho kusudia ? Inaweza ikafika lakini je, ni kwa kiwango standard ?
Free Advice/ Ushauri

1. Anza kufuatilia report za kiuchumi za World bank & IMF

2. Soma Majarida ya uwekezaji ya kimataifa

3. Soma Historia za watu waliofanikiwa sana kiuwekezaji

4. Jifunze kutengeneza mikakati/Strategies ( Angalia Clip za video za kijeshi mfano Vita ya Marekani na Japan, Israel na Misri na washilika wake, Jifunze jinsi mikakati inavyo andaliwa.
Tukutane wakati ujao !!!!

Comments

Popular posts from this blog

Hatua tisa za kuanzisha biashara.

Kuanzisha biashara kunahitaji kupanga mipango, kufanya maamuzi ya kifedha  na kutimiza  taratibu kadhaa za kisheria.  Wakati mwingine sio lazima kuzifanya  hatua zote kwa wakati mmoja lakini kadri biashara inavyozidi kuimarika basi ni lazima uzitimize hizo hatua muhimu. Kuna baadhi ya hatua ambazo ni lazima uzifanye mwanzoni kabisa mwa biashara yako, vinginevyo biashara yako itakufa ingali bado changa au itasimamishwa na mamlaka husika za kisheria. Hatua zifuatazo zawaeza kukusaidia katika kupanga,kujiandaa na kuingoza biashara yako kwa ufanisi mkubwa zaidi: Andaa mwongozo wa biashara ( Business plan) Mwongozo huu utakusaidia  kukupa dira ya namna ya kuanza na kuendesha biashara yako kwa ufanisi. Tafuta msaada na mafunzo ya kibiashara Tumia fursa za bure za kujifunza  zinazopatikana mtandaoni au fursa za bei rahisi zinazotolewa katika makongamano ya ujasiriamali na uwekezaji hapa nchini. Chagua eneo sahihi la kuiweka biashara yako. Tafuta us

Mambo muhimu kuhusu mkopo - Sehemu ya 1

            Utangulizi  MKOPO ni kiwango cha fedha ambacho mtu hupewa na taasisi ya kifedha na kutakiwa kurudisha kiwango hicho kikiwa na riba kwa kipindi cha muda fulani. Mkopo unaweza  kuwa katika  mfumo wa bidhaa au kifaa lakini vitu hivyo  vyote hatimaye lazima thamani yake ipimwe na fedha,kwasababu  kazi kubwa ya fedha ni kupima thamani ya bidhaa au vifaa,mfano mtu anapochukua mkopo wa bidhaa zenye thamani ya Milioni kumi,tafsiri  yake ni kwamba umechukua mkopo wa Milioni kumi. Katika makala hii nitaeleza kuhusu mkopo kwa ujumla ingawa kwa sehemu kubwa nitaeleza juu ya mkopo wa fedha  unaotolewa na taasisi za za kifedha. Watu wamezoea kuwa mabenki ndiyo yanayo husika na utoaji wa mikopo tu lakini kiuhalisia kuna taasisi nyingi za kifedha zinazo husika na utoaji wa mikopo . Kulingana na sheria ya benki na taasisi za kifedha vyombo ambayo vinaruhusiwa na huduma ya utoaji mikopo ni benki ,saccos ,makampuni ya mikopo na mifuko ya hifadhi ya jamii. Tafiti zinaonyes

Mambo sita ya msingi kuhusu soko la bidhaa yako au huduma unayotoa

Sokoni ni eneo ambalo wauzaji wa bidhaa na wanunuzi wa bidhaa hukutana kubadilisha thamani vitu. Katika nyakati hizi soko la bidhaa linaweza kuwa ni kwa njia ya mtandao hivyo sio lazima mnunuzi na muuzaji wa bidhaa kukutana uso kwa uso. Kipindi hiki ni zama za sayansi na teknolojia ambazo zimetoa matumizi makubwa ya mtandao katika shughuli za mwanadamu hususani biashara hivyo kuna biashara nyingi zinafanyika kwenye mtandaoni (Online). Ninaamini wengi wetu tumeingia katika shughuli za ujaseriamali kwa dhumuni la kuongeza kipato hatimaye kuwa na maisha mazuri. Hivyo basi swala la soko katika biashara yako ni muhimu sana kwasababu bidhaa unazozalisha ni kwaajili ya kuuza na kupata faida.Katika biashara ya aina yoyote mzalishaji hana budi afahamu mambo kadhaa ya msingi kuhusu soko la bidhaa yake au huduma na kisha  kumsaidia kufanya maamuzi ya kumuwezesha kupata faida ya juu katika biashara anayoifanya. 1.Unahitaji kufanya utafiti wa kina juu ya soko la bidhaa z