Sokoni ni eneo ambalo wauzaji wa bidhaa na wanunuzi wa bidhaa hukutana
kubadilisha thamani vitu.
Katika nyakati hizi soko la bidhaa linaweza kuwa ni kwa njia ya
mtandao hivyo sio lazima mnunuzi na muuzaji wa bidhaa kukutana uso kwa uso.
Kipindi hiki ni zama za sayansi na teknolojia ambazo zimetoa
matumizi makubwa ya mtandao katika shughuli za mwanadamu hususani biashara
hivyo kuna biashara nyingi zinafanyika kwenye mtandaoni (Online).
Ninaamini wengi wetu tumeingia katika shughuli za ujaseriamali
kwa dhumuni la kuongeza kipato hatimaye kuwa na maisha mazuri.Hivyo basi swala la soko katika biashara yako ni muhimu sana kwasababu
bidhaa unazozalisha ni kwaajili ya kuuza na kupata faida.Katika biashara ya
aina yoyote mzalishaji hana budi afahamu mambo kadhaa ya msingi kuhusu soko la
bidhaa yake au huduma na kisha kumsaidia
kufanya maamuzi ya kumuwezesha kupata faida ya juu katika biashara anayoifanya.
1.Unahitaji
kufanya utafiti wa kina juu ya soko la bidhaa zako ilikujua ni bidhaa gani
inayohitajika sokoni ?.Utafiti ndio utakao kupa jawabu la aina ya bidhaa ambayo
inahitajika sokoni hivyo kama mjasiriamali usikurupuke tuu bila kuwa na uhakika
wa aina ya bidhaa au huduma ambayo inahitajika sokoni.
2.Je
soko la bidhaa yako ni wapi na hali ya miundombinu za kulifikia iko vipi pia
itakusaidia ufahamu gharama ya kufika sokoni kama utaamua kuuzia sokoni ,kama
bidhaa yako itakuwa inauzika katika eneo la uzalishaji inamaana swala la gharama
za usafirishaji utaliepeuka lakini kwa mjasiriamali ambaye hazalishi bidhaa kwake
swala la gharama ya usafiri wa kupeleka bidhaa yake sokoni ni muhimu sana
kulifahamu.Mfano kama unanunua alizeti Singida ni vizuri kujua gharama ya
usafiri kutoka Singida kwenda kwenye soko husika la hiyo bidhaa.
3.Bidhaa
inahitajika kwa wingi kiasi gani na wakati gani sokoni ni vizuri kufahamu mambo
hayo mawili muhimu ilikuepeka na uzalishaji mwingi ambao utapelekea kushusha
bei ya bidha yako na kupunguza faida pili ni kuzalisha bidhaa yako sawasawa na
majira ya soko mfano huwezi kuuza masweta na makoti wakati wa joto hivyo
itakulazimu kusubiri nyakati za baridi kwasababu mzunguko wa bidhaa hizo huwa
ni mkubwa wakati huo.
4.Soko
linahitaji bidhaa yenye sifa zipi,siku zote mfanya biashara huwa anazalisha
bidhaa zenye kukidhi matakwa ya mteja sokoni hivyo ni vizuri kufahamu wateja
wako ni kina nani na je wanahitaji bidhaa zenye ubora gani ? .Mfano kama wateja
wako ni wanawake ni lazima bidhaa yako iendane na mahitaji yao kwa wakati huo
(fashion).
5.Kama
wanunuzi watakuwa na utayari kununulia unakozalishia, je unao uwezo wakutosheleza
mahitaji yao wewe pekee yako .Kama huwezi kukidhi kiwango ili uweze kujipanga
kukidhi mahitaji kwa kuongeza uzalishaji au kwa kuungana na wazalishaji wengine.
6.Linganisha
bei ya bidhaa sokoni na bei ya kuuzia unakozalishia (ili ujue palipo na faida zaidi
kwako baada ya kuondoa gharama ya kupeleka bidhaa zako sokoni ) Ila ukiamua
kuuzia sokoni hakikisha unakuwa na uwezo
wa kushindana na wauzaji wengine huko sokoni katika ubora wa bidhaa na wakati
mwingine ushindani katika bei ya bidhaa .
Comments
Post a Comment