Skip to main content

Mambo Muhimu Kuhusu Soko

 Mambo muhimu kuhusu mikopo kabla ya kuchukua mkopo katika taasisi za kifedha.

Zifuatazo ni dondoo muhimu kuhusu mikopo.

1.Dhumuni lako ni nini

Ni vizuri ukajihoji binafsi unachukua mkopo kwaajili ya kufanyianin?.

Jambo la ajabu na la kusikitisha endapo utachukua mkopo kwa ajili ya matumizi ya kawaida mfano kununulia nguo,chakula na kadhalika.

Chukua mkopo kwa dhumuni la kufanyia biashara yaani chukua fedha ili uzalishe fedha.

2.Je ni kiwango gani cha fedha kinaweza kukidhi haja ya biashara yako au thamani unayohitaji kununua

Unahitaji kiwango gani cha fedha  unapokwenda katika taasisi za kifedha kama benki na saccos moja kati ya swali muhimu ambalo utaulizwa ni kiwango gani cha fedha unahitaji?.

Awali, kuwa na mpango kazi(Business Plan) wa biashara yako ambayo imebeba mchanganuo wa biashara yako kwa kina.

Mpango kazi wenyewe uwe na uwezo wa kujibu maswali mengi ambayo taasisi za kifedha zitakuuliza.

3.Je unathamani ambayo unaweza kuweka rehani kulinda huo mkopo endapo utashindwa kulipa?( mfano wa thamni hizo ni Nyumba ,kiwanja au shamba)

Taasisi za kifedha huwa wanahitaji uwe na thamani ya kuweka rehani kwa ajili ya mkopo unaotaka kuchukua ili fedha zao ziwe katika mazingira salama endapo utashindwa kulipa.

Kwa watu ambao ni waajiriwa huwa inahitajika barua ya mwajiri na pia awe mteja wa benki husika mwenye akaunti ya mshahara katika hiyo benki.

Tena baadhi ya taasisi za kifedha ambazo zinaweza kukupa fedha bila kuwa mteja kwao lakini ni lazima udhaminiwe na mteja ambaye ana akaunti katika taasisi husika.

4.Je unauwezo wa kurejesha mkopo kwa muda gani? 

Ni vizuri kufahamu kipindi ambacho fedha hiyo inapaswa kurudi katika taasisi husika ili ujue kama kwa kipindi hicho utakuwa na uwezo wa kulipa mkopo huo. .

Unapokwenda katika taasisi za kifedha kwa dhumini la kuchuka mkopo uliza.

Comments

Popular posts from this blog

Hatua tisa za kuanzisha biashara.

Kuanzisha biashara kunahitaji kupanga mipango, kufanya maamuzi ya kifedha  na kutimiza  taratibu kadhaa za kisheria.  Wakati mwingine sio lazima kuzifanya  hatua zote kwa wakati mmoja lakini kadri biashara inavyozidi kuimarika basi ni lazima uzitimize hizo hatua muhimu. Kuna baadhi ya hatua ambazo ni lazima uzifanye mwanzoni kabisa mwa biashara yako, vinginevyo biashara yako itakufa ingali bado changa au itasimamishwa na mamlaka husika za kisheria. Hatua zifuatazo zawaeza kukusaidia katika kupanga,kujiandaa na kuingoza biashara yako kwa ufanisi mkubwa zaidi: Andaa mwongozo wa biashara ( Business plan) Mwongozo huu utakusaidia  kukupa dira ya namna ya kuanza na kuendesha biashara yako kwa ufanisi. Tafuta msaada na mafunzo ya kibiashara Tumia fursa za bure za kujifunza  zinazopatikana mtandaoni au fursa za bei rahisi zinazotolewa katika makongamano ya ujasiriamali na uwekezaji hapa nchini. Chagua eneo sahihi la kuiweka biashara yako. Tafuta us

Mambo muhimu kuhusu mkopo - Sehemu ya 1

            Utangulizi  MKOPO ni kiwango cha fedha ambacho mtu hupewa na taasisi ya kifedha na kutakiwa kurudisha kiwango hicho kikiwa na riba kwa kipindi cha muda fulani. Mkopo unaweza  kuwa katika  mfumo wa bidhaa au kifaa lakini vitu hivyo  vyote hatimaye lazima thamani yake ipimwe na fedha,kwasababu  kazi kubwa ya fedha ni kupima thamani ya bidhaa au vifaa,mfano mtu anapochukua mkopo wa bidhaa zenye thamani ya Milioni kumi,tafsiri  yake ni kwamba umechukua mkopo wa Milioni kumi. Katika makala hii nitaeleza kuhusu mkopo kwa ujumla ingawa kwa sehemu kubwa nitaeleza juu ya mkopo wa fedha  unaotolewa na taasisi za za kifedha. Watu wamezoea kuwa mabenki ndiyo yanayo husika na utoaji wa mikopo tu lakini kiuhalisia kuna taasisi nyingi za kifedha zinazo husika na utoaji wa mikopo . Kulingana na sheria ya benki na taasisi za kifedha vyombo ambayo vinaruhusiwa na huduma ya utoaji mikopo ni benki ,saccos ,makampuni ya mikopo na mifuko ya hifadhi ya jamii. Tafiti zinaonyes

Mambo sita ya msingi kuhusu soko la bidhaa yako au huduma unayotoa

Sokoni ni eneo ambalo wauzaji wa bidhaa na wanunuzi wa bidhaa hukutana kubadilisha thamani vitu. Katika nyakati hizi soko la bidhaa linaweza kuwa ni kwa njia ya mtandao hivyo sio lazima mnunuzi na muuzaji wa bidhaa kukutana uso kwa uso. Kipindi hiki ni zama za sayansi na teknolojia ambazo zimetoa matumizi makubwa ya mtandao katika shughuli za mwanadamu hususani biashara hivyo kuna biashara nyingi zinafanyika kwenye mtandaoni (Online). Ninaamini wengi wetu tumeingia katika shughuli za ujaseriamali kwa dhumuni la kuongeza kipato hatimaye kuwa na maisha mazuri. Hivyo basi swala la soko katika biashara yako ni muhimu sana kwasababu bidhaa unazozalisha ni kwaajili ya kuuza na kupata faida.Katika biashara ya aina yoyote mzalishaji hana budi afahamu mambo kadhaa ya msingi kuhusu soko la bidhaa yake au huduma na kisha  kumsaidia kufanya maamuzi ya kumuwezesha kupata faida ya juu katika biashara anayoifanya. 1.Unahitaji kufanya utafiti wa kina juu ya soko la bidhaa z