Skip to main content

MUONGOZO WA KUANZISHA VIKUNDI VYA UJASIRIAMALI

 

                                                                 UTANGULIZI










Mfululizo wa makala hizi ni mahususi kwaajili ya kujenga uelewa utakaosaidia wajasiriamali katika kuanzisha vikundi vya ujasiriamali. 

Kumekuwepo na changamoto katika kuanzisha vikundi vya ujasirimali  na hii ni kutokana na kukosa ufahamu sahihi katika namna ya kuanzisha na kuendesha shughuli za vikundi vya ujasiriamali.  

Jamii inapaswa kujua umuhimu wa kufanya biashara katika mfumo wa vikundi vya ujasiriamali ili kuona hitaji la kuanzisha vikundi vya ujasiriamali katika maeneo yao na sio taasisi kuanzisha vikundi vya ujasiriamali kwasababu jamii isiposhiriki katika uanzishwaji wa kikundi kuna uwezekano mkubwa wa kikundi kuanzishwa ambacho hakina uwezo wa kusaidia wanakikundi kujenga uwezo wa  kujitegemea kiuchumi. 


Moja ya sababu ambayo ilichangia taifa la Tanzania kuingia miongoni mwanchi zenye kipato cha kati ni ukuaji wa uchumi mkubwa ambao unajumuisha sekta zote za uzalishaji na wajasiriamali ni kundi muhimu sana kama sehemu ya uzalishaji hivyo ubora wa vikundi vya ujasirimali vinamchango chanya katika maendeleo na ukuaji wa uchumi. Faida ambazo tunaweza kuzipata kwa kuwa na vikundi bora vya ujasiriamali. 

i) Upatikanaji wa ajira
ii) Chanzo cha kipato kupitia kodi na tozo mbalimbali mfano ushuru na zinginenezo
iii) Upatikanaji wa dhamana katika taasisi za kifedha
iv) Ongezeko la mtaji kwa wajasiriamali

Itaendelea 


Imeandaliwa na James Albert 
Simu 0717162510
Barua pepe jamesalbert157@gmai.com






















Comments

Popular posts from this blog

Hatua tisa za kuanzisha biashara.

Kuanzisha biashara kunahitaji kupanga mipango, kufanya maamuzi ya kifedha  na kutimiza  taratibu kadhaa za kisheria.  Wakati mwingine sio lazima kuzifanya  hatua zote kwa wakati mmoja lakini kadri biashara inavyozidi kuimarika basi ni lazima uzitimize hizo hatua muhimu. Kuna baadhi ya hatua ambazo ni lazima uzifanye mwanzoni kabisa mwa biashara yako, vinginevyo biashara yako itakufa ingali bado changa au itasimamishwa na mamlaka husika za kisheria. Hatua zifuatazo zawaeza kukusaidia katika kupanga,kujiandaa na kuingoza biashara yako kwa ufanisi mkubwa zaidi: Andaa mwongozo wa biashara ( Business plan) Mwongozo huu utakusaidia  kukupa dira ya namna ya kuanza na kuendesha biashara yako kwa ufanisi. Tafuta msaada na mafunzo ya kibiashara Tumia fursa za bure za kujifunza  zinazopatikana mtandaoni au fursa za bei rahisi zinazotolewa katika makongamano ya ujasiriamali na uwekezaji hapa nchini. Chagua eneo sahihi la kuiweka biashara yako. Tafuta us

Mambo muhimu kuhusu mkopo - Sehemu ya 1

            Utangulizi  MKOPO ni kiwango cha fedha ambacho mtu hupewa na taasisi ya kifedha na kutakiwa kurudisha kiwango hicho kikiwa na riba kwa kipindi cha muda fulani. Mkopo unaweza  kuwa katika  mfumo wa bidhaa au kifaa lakini vitu hivyo  vyote hatimaye lazima thamani yake ipimwe na fedha,kwasababu  kazi kubwa ya fedha ni kupima thamani ya bidhaa au vifaa,mfano mtu anapochukua mkopo wa bidhaa zenye thamani ya Milioni kumi,tafsiri  yake ni kwamba umechukua mkopo wa Milioni kumi. Katika makala hii nitaeleza kuhusu mkopo kwa ujumla ingawa kwa sehemu kubwa nitaeleza juu ya mkopo wa fedha  unaotolewa na taasisi za za kifedha. Watu wamezoea kuwa mabenki ndiyo yanayo husika na utoaji wa mikopo tu lakini kiuhalisia kuna taasisi nyingi za kifedha zinazo husika na utoaji wa mikopo . Kulingana na sheria ya benki na taasisi za kifedha vyombo ambayo vinaruhusiwa na huduma ya utoaji mikopo ni benki ,saccos ,makampuni ya mikopo na mifuko ya hifadhi ya jamii. Tafiti zinaonyes

Mambo sita ya msingi kuhusu soko la bidhaa yako au huduma unayotoa

Sokoni ni eneo ambalo wauzaji wa bidhaa na wanunuzi wa bidhaa hukutana kubadilisha thamani vitu. Katika nyakati hizi soko la bidhaa linaweza kuwa ni kwa njia ya mtandao hivyo sio lazima mnunuzi na muuzaji wa bidhaa kukutana uso kwa uso. Kipindi hiki ni zama za sayansi na teknolojia ambazo zimetoa matumizi makubwa ya mtandao katika shughuli za mwanadamu hususani biashara hivyo kuna biashara nyingi zinafanyika kwenye mtandaoni (Online). Ninaamini wengi wetu tumeingia katika shughuli za ujaseriamali kwa dhumuni la kuongeza kipato hatimaye kuwa na maisha mazuri. Hivyo basi swala la soko katika biashara yako ni muhimu sana kwasababu bidhaa unazozalisha ni kwaajili ya kuuza na kupata faida.Katika biashara ya aina yoyote mzalishaji hana budi afahamu mambo kadhaa ya msingi kuhusu soko la bidhaa yake au huduma na kisha  kumsaidia kufanya maamuzi ya kumuwezesha kupata faida ya juu katika biashara anayoifanya. 1.Unahitaji kufanya utafiti wa kina juu ya soko la bidhaa z